Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (WAMJW),
imepata kibali cha ajira 547 kutoka Ofisi ya Rais – UTUMISHI za
Wataalamu wa kada mbalimbali za Afya wanaokidhi vigezo vya kuaajiriwa
chini ya Wizara ya Afya na Taasisi zake.
Huu ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita
inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mama Samia Suluhu Hassan.
Ajira 547 inajumulisha nafasi 473 ambazo zitaratibiwa na WAMJW wakati
nafasi 74 zitakaratibiwa na Sekretariati ya ajira. Wataalamu 74 wa kada
mbalimbali wataajiriwa katika Maabara Kuu ya Taifa; na wataalamu 473 wa
kada mbalimbali wataajiriwa katika Hospitali za Kanda za KCMC, Mbeya,
Bugando na Benjamini Mkapa, Hospitali za Rufaa za Mikoa na vyuo
mbalimbali vilivyopo chini ya WAMJW.
Watalaamu 473 chini ya uratibu wa WAMJW ambao watanufaika na nafasi
hizi ni pamoja na; Madaktari wauguzi, Wafamasia, Wateknolojia wa Dawa,
Wateknolojia wa Maabara, Wateknolojia wa Mionzi, Wateknolojia wa
Macho, Watoa Tiba kwa Vitendo, Maafisa Afya Mazingira, Wasaidizi wa
Afya, Makatibu Afya, Maafisa Ustawi wa Jamii na Maafisa Lishe.
Telegrams “AFYA”, DODOMA
Nambari ya simu: +255-026-2323267/2351196
Nukushi Na: +255-22-213806
Mji wa Serikali - Mtumba,
Barabara ya Afya,
S. L. P 743,
40478 DODOMA.
Ajira hizo (473) zitajaza nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliokoma
utumishi kutokana na sababu mbalimbali. Waombaji wanasisitizwa
kuzingatia maelekezo yote yatakayotolewa na vyanzo rasmi vya taarifa za
ajira na utaratibu kupitia tovuti www.moh.go.tz kwa kiunganishi
(ajira.moh.go.tz). Maombi ni kuanzia tarehe 12 hadi 25 Mei, 2021.
🔘JE, NA WEWE UNA HABARI?
🔘WASILIANA NA MwanaHALISI TV ( +255 767 400402),
🔘WhatsApp ( +255 692 318213)
🔘Email: mwanahalisitvnews@gmail.com
🔘KWA HABARI ZA KILA SIKU: http://mwanahalisionline.com